Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, wabunge Chadema ‘waliamsha dude’ ofisi za Tume
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, wabunge Chadema ‘waliamsha dude’ ofisi za Tume

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema (katikati) akiwa na Mgombea Ubunge Kinondoni, Salum Mwalimu walipowasili ofisi za NEC
Spread the love

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiongozana na Mgombea Ubunge Jimbo la Kinodnoni, Salumu Mwalimu pamoja na wabunge wa Chadema katika ofisi za Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC) kuhoji sababu za mawakala wake kutopewa hati za viapo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mbowe akiongozana na wenzake amelazimika kufika katika ofisi hizo kwa lengo la kuhoji sababu zilizofanya mawakala wa Uchaguzi Jimbo la Kinondoni wasipewa nakala za viapo hadi leo huku ikiwa uchaguzi unatarajiwa kufanyika Februari 17, mwaka huu.

Mwenyekiti huyo pamoja na kuongozana na Mwalimu, mgombea ubunge wa jimbo hilo, pia ameongozana na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini na mwanachama wengine wa chama hicho.

“Tumekuja Tume kuonana na Mkurugenzi wa Tume Taifa juu ya hujuma zinazofanywa na Mkurugenzi wa Kinondoni kwa kutowapa mawakala wetu nakala za kiapo mpaka sasa hivi,” amesema Mbowe.

Lakini pamoja na Mbowe na wenzake kufika ofisini hapo, wameambiwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Ramadhani Kailima hayupo ofisini na wameahidi kuendelea kubaki mpaka atakaporudi ofisini.

MwanaHALISI Online itaendelea kuwapa taarifa nini kinachopendelea katika ofisi za NEC.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!