Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, Matiko waitwa Mahakama ya Rufaa
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, Matiko waitwa Mahakama ya Rufaa

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko wakiwa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam
Spread the love

KESI ya kupinga kurejeshewa dhamana iliyofunguliwa na serikali dhidi ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasim na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na Mwekahazina wa Baraza la Wanawake la chama hicho (BAWACHA), Esther Matiko, itasikilizwa Mahakama ya Rufaa jijini Dar es Salaam, tarehe 18 Februari mwaka huu. Anaripoti Yusuph Katimba … (endelea).

Serikali iliwasilisha Mahakama ya Rufaa, maombi ya kuwazuia Mbowe na Matiko kurejeshewa dhamana zao. Ni baada ya Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, kutupilia mbali mapingamizi ya serikali yaliyotaka mahakama hiyo kutosikiliza shauri lililofunguliwa na Mbowe na Matiko.

Kwa mujibu wa vyanzo via taarifa kutoka Mahakama ya Rufaa na ambazo zimethibitishwa na Prof. Abdallah Safari, ambaye anaongoza jopo la mawakili katika kesi hiyo, ni kwamba “Mbowe na Matiko, watafika mbele ya majaji wa mahakama ya rufaa, Jumatatu ya tarehe 18 Februari.”

Mbowe ambaye pia ni mbunge wa Hai, mkoani Kilimanjaro na Kiongozi wa Kambi rasmi ya upinzani bungeni, alifutiwa dhamana na mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa madai ya kukiuka masharti ya dhamana aliyopewa.

Katika uamuzi wake, mahakama ilisema, maelezo yaliyotolewa na Mbowe, mdhamini wake na wakili wake, yalilenga kuidanganya mahakama.

Naye Matiko ambaye pia ni mbunge wa Tarime Mjini, alifutiwa dhamana na mahakama baada ya kushindwa kufika mahakamani kwa mara mobile mfululizo kwa maelezo kuwa alikuwa nje ya nchi kwa shughuli za Bunge.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!