Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe kuongoza kikao cha ‘machinjio’
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe kuongoza kikao cha ‘machinjio’

Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anatarajia kuongoza kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho, cha kuteua wagombea wa nafasi mbalimbali za mabaraza. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Mabaraza hayo ni pamoja na Baraza la Wazee Chadema (Bazecha), Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) na Baraza la Vijana Chadema (Bavicha).

Taarifa iliyotolewa Tumaini Makene, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Chadema tarehe 6 Desemba 2019, inaeleza kikao hicho kitaketi kwa siku moja (Jumamosi) kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.

“Kamati Kuu ya chama itakutana kwa siku moja katika kikao chake cha kikatiba ambapo agenda kuu, itakuwa uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali za uchaguzi wa mabaraza ya chama. Kikao hicho kitakuwa chini ya Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mbowe,” inaeleza taarifa ya Makene.

Taarifa hiyo imeeleza zaidi kuwa, baada ya kikao hicho kuketi, Chadema itatoa taarifa kwa umma kuhusu majina ya watakaoteuliwa kuendelea na mchakato wa uchaguzi.

Chadema inatarajia kufanya uchaguzi wa viongozi wake wa kitaifa tarehe 18 Desemba 2019. Ambapo kwa sasa, uchaguzi wa viongozi wa chama hicho wa kanda, umeshafanyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

error: Content is protected !!