Friday , 29 March 2024
Habari za Siasa

Mbowe awindwa Hai

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anawindwa jimboni kwake Hai, Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mwita Waitara, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), amemwelekeza Lengai Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai kufuata fedha za mfuko wa Jimbo la Hai na kupanga matumizi.

Amesema, fedha hizo Sh. 42 milioni zipo kwa Mbowe tangu mwaka 2018/19 na hazijapangiwa matumizi, na sasa miaka miwili imepita bila kutumika.

Akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, tarehe 8 Januari 2020, Waitara amesema, mwenye mamlaka ya kupanga matumizi ya fedha hizo si Mbowe bali ni Mkuu wa Wilaya na mkurugenzi.

Mwita amemtaka Sabaya kumwagiza mkurugenzi wa halmashauri hiyo kufanya utaratibu wa kupata fedha na kupanga matumizi yake naye (Sabaya) kusimamia.

Pia amemtuhumu Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai, kwamba amekuwa mtoro na hafanyi kazi za jimbo, na amekuwa akifanya matumizi ya fedha hizo kwa njia ya simu, kitu ambacho hakikubaliki.

MwanaHALISI Online leo tarehe 9 Januari 2020, limemtafuta Mbowe ili kupata ufafanuzi kuhusu tuhuma hizo bila mafanikio. Na hata alipoandikiwa ujumbe mfupi wa maneno, hajajibu.

Kwenye mkutano huo, Sabaya amemuahidi Mwita kwamba, hakuna fedha zitazochezewa na kwamba, yoyote atakayejaribu kufanya hivyo, atamfyatua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!