Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe awaangukia viongozi wa dini
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe awaangukia viongozi wa dini

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amewaomba viongozi wa dini kuliombea taifa, ili liwe salama kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Pwani … (endelea).

Mbowe ametoa wito huo kwenye ibada maalumu ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Mzee Elias Mwingira,  Baba wa Nabii na Mtume wa Kanisa  la Huduma ya Efatha, Josephat Mwingira, leo tarehe 22 Februari 2020, Kibaha mkoani Pwani.

Kiongozi huyo wa Chadema amewaomba viongozi wa dini zote nchini, kuungana kwa pamoja katika kumuomba Mungu, ili uchaguzi huo ufanyike kwa amani.

“Ombi langu maalum kwako Nabii na Mtume Josephat Mwingira, wewe na viongozi wengine kutoka dini zote, mkaungane kuliombea taifa katika mwaka huu wa uchaguzi,” ameomba Mbowe.

Wakati huo huo, Mbowe amewaomba viongozi wa dini kuwaombea viongozi wa vyama siasa ili Mungu awape unyenyekevu.

“Pia mkatuombee sisi  Viongozi wa kisiasa tuache viburi, tuvae unyenyekevu, tukawe na tume huru ya uchaguzi katika uchaguzi ujao, haki ikatamalaki” amesema Mbowe.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!