Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe ‘apinduliwa’ bungeni
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe ‘apinduliwa’ bungeni

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

WABUNGE 12 kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), waliorejea bungeni kabla ya muda waliokubaliana na wenzao kumalizika, wameunda uongozi wao bungeni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa kutoka ndani ya ofisi ya Katibu wa Bunge mjini Dodoma zinasema, kambi hiyo mpya ya upinzani, inaongozwa na Mbunge wa Bukoba Mjini, Willifred Muganyizi Lwakatare.

Akizungumza na MwanaHALISI mmoja wa wabunge waliorejea bungeni amesema, wameamua kuchukua hatua hiyo, ili kurahisisha kazi zao na kuwa na mawasiliano ya uhakika na ofisi ya Spika.

“Ni kweli, sisi tuliyobaki bungeni, tumeamua kuunda uongozi wetu. Tumemchagua Lwakatare kuwa kiongozi wetu (KUB). Na kesho tunakwenda kwa Spika Ndugai, ili kumtaarifu,” ameeleza.

Lwakatare ni mmoja wa wabunge wa Chadema walioamua kurejea bungeni, kupinga maagizo ya mwenyekiti wao, Freeman Mbowe.

Wilfred Lwakatare, Mbunge wa Bukoba Mjini

Kambi ya Lwakatare imeundwa kuchukua nafasi ya ile iliyokuwa inaongozwa na Freeman Mbowe, ambaye kwa sasa yuko nje ya Bunge akijitenga na maambukizi ya Corona.

Wengine waliochaguliwa kuunda uongozi wa kambi hiyo, ni Latifa Chande ambaye anakuwa katibu na Anthony Komu, aliyefanywa kuwa Mnadhimu wa kambi hiyo.

Viongozi hao watatu ndio watakaongoza kambi ya upinzani bungeni hadi hapo Freeman na wenzake watakaporuhusiwa kurejea bungeni.

Hata hivyo Lwakatale, alipoulizwa kuhusiana na taarifa hizo, amekana madai hayo na kueleza kuwa walichounda wao, ni uongozi wa muda wa kuwasaidia kufanikisha shughuli zao.

Alisema, “tulichounda jana, ni uongozi wa muda ambako tumeteuwa Mmadhimu wa Kambi ya Upinzani ambaye atakuwa na kazi ya kutusaidia kutuunganisha pamoja.”

Aliongeza: “Hatujampindua mwenyekiti na hatuko hapa kumpindua yeyote. Tuko bungeni kuwakilisha wananchi na ili tufanye kazi hiyo, sharti tuwe na uongozi. Hilo ndilo tulilolifanya.”

Spika wa Bunge, Job Ndugai alitangaza jana Jumanne kuwa wabunge wa Chadema wasiporejea bungeni hadi kumalizika siku 14 walizojipa, hawataruhusiwa kuingia bungeni, hadi hapo watakapopima afya zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!