Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Chakula cha sumu chauwa Watu 24 wa familia moja
Kimataifa

Chakula cha sumu chauwa Watu 24 wa familia moja

Spread the love

 

WATU 24 wa familia moja wamefariki dunia nchini Nigeria, baada ya kula chakula chenye sumu. Inaripoti BBC … (endelea).

Taarifa ya tukio hilo imetolewa jana Jumanne na Kamishna wa Afya wa Jimbo la Sokoto, nchini humo, Ali Inname, akizungumza na waandishi wa habari.

Inname alisema, watu hao walikula chakula chenye sumu ya mbolea aina ya Gishirin Lalle, iliyowekwa katika chakula hicho kimakosa, wakidhani ni chumvi.

Kamishna huyo wa afya, alisema tukio hilo lilitokea Jumatatu, tarehe 9 Agosti 2021.

Hata hivyo, alisema wanafamilia wawili walinusurika kifo kwa kuwa hawakula chakula kingi. Watu hao wanapatiwa matibabu hospitalini.

Inname alishauri wananchi kutenganisha vyakula na vitu vyenye sumu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!