Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbatia: Nimemuuliza rais, nchi hii tunaipeleka wapi?
Habari za Siasa

Mbatia: Nimemuuliza rais, nchi hii tunaipeleka wapi?

Spread the love

JAMES Mbatia, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi amesema amekutana na Rais John Magufuli na kumuuliza, hatima ya Tanzania. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 3 Machi 2020, katika Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam, Mbatia amesema Rais Magufuli aliwawaita wapinzani ili kuzungumzia masuala ya mbalimbali ya kitaifa.

“Leo nimeitwa na rais, alikuwa anaongea na viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa. Nikamuuliza, nchi hii tunaipaleka wapi?

“Akaniambia, anaendelea kusisitiza, uchaguzi wa mwaka huu utakuwa huru na haki, kama vyama vya siasa tukae chini tuzungumze tuweke kanuni sheria na utaratibu,” amesema.

Amesema, ametumia nafasi hiyo kumkumbusha rais kuhusu masuala ya maridhiano, masuala ya Watanzania na wadau wa siasa kukaa pamoja na kutosahau kwamba binadamu wote ni ndugu.

Hata hivyo, Mbatia ameeleza kusikitishwa na namna yeye na chama chake wanavyoporomoshewa matusi kutokana na itikadi ya chama hicho ya utu.

Mbatia amedai, watu wanaomtukana pamoja na chama hicho ni wale ambao wanapingana na fikra za NCCR-Mageuzi, na kuwa hawatojibu matusi hayo kwani chama hicho kina haki ya kuwa na fikra tofauti na wengine.

“Yameanza kutokea matusi ya yanayo dhalilisha sana, natukanwa sana lakini kama ni matusi hayanipi shida sana, leo tunatukanana na hakuna wakukemea matusi haya, tuna haki ya kuwa na fikra tofauti na wengine,” amesema na kuongeza:

“Wale ambao wanajaribu kwenda kinyume na msimamo wetu wa itikadi yetu ya utu, ni bahati mbaya sana na inasikitisha japo wanatutukana wao kwasababu ya itikadi yetu ya utu, sisi hatutawarudishia matusi. Tutazungumzia misingi endelevu ya kuliunganisha taifa letu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!