Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mawaziri wanne wakatwa ubunge 
Habari za Siasa

Mawaziri wanne wakatwa ubunge 

Dk. Harisson Mwakyembe
Spread the love

MAWAZIRI wanaohudumu kwenye utawala wa awamu ya tano chini ya Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli ‘wamekatwa’ kwenye mchakato wa kuwania ubunge ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Jana Alhamisi tarehe 20 Agosti 2020, Halmashauri Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti wake, Rais Magufuli ilihitimisha safari ya mwezi moja na nusu ya kupata wagombea ubunge wa majimbo na viti maalum.

Katika uteuzi uliofanywa na kikao hicho, ulionyesha wateule wa Rais Magufuli kwenye baraza lake, mawaziri wawili na naibu mawili wawili wameangukia pua.

Mawaziri kamili ni, Dk. Harisson Mwakyembe wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Angellah Kairuki wa Ofisi ya Waziri Mkuu- Uwekezaji.

Angellah Kairuki wa Ofisi ya Waziri Mkuu- Uwekezaji

Pia, kuna naibu mawaziri, Omary Magumba wa Kilimo na Dk. Mary Mwanjelwa wa Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Dk. Makyembe ameshindwa kutetea nafasi yake ya ubunge Kyela Mkoa wa Mbeya ambapo aliyeteuliwa ni Ally Jumbe.

Waziri mwingine ni Angellah Kairuki wa Uwekezaji.

Kairuki alikuwa mbunge wa viti maalum ambaye katika mchakato wa uchaguzi mwaka huu, alikwenda kugombea jimbo la Same Magharibi.

Omary Magumba, Naibu Waziri wa Kilimo

Aliyeteuliwa ni Dk. Mathayo David ambaye aliongoza kura za kaoni katika harakati zake za kutetea jimbo hilo alilokuwa akiliongoza.

Omary Mgumba, naibu waziri wa kilimo, yeye ameshindwa kutetea nafasi yake jimbo la Morogoro Kusini Mashariki.

Safari ya Mgumba ilianza kuingia doa baada ya Hamis Shabani maarufu Babu Tale, Meneja wa mwanamuziki nchini Diamond Platinum kumshinda kura za maoni na hatimaye kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi mkuu.

Dk. Mary Mwanjelwa, Naibu Waziri wa Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Dk. Mary Mwanjelwa, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora aliyekuwa akiwanua viti maalum mkoa wa Mbeya, amejikuta akiangukia pua licha ya kuongoza katika kura za maoni.

3 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!