Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mawaziri hawa hawako salama
Habari za Siasa

Mawaziri hawa hawako salama

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (kushoto). Picha ndogo, Charles Tizeba, Waziri wa Kilimo
Spread the love

WAZIRI wa Kilimo, Charles Tizeba na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina siku zao zinahesabika kutokana kushindwa kuhudhuria bila kutoa taarifa kwenye Mkutano ulioitwa na Rais Jonh Magufuli. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mkutano huo uliwakutanisha wafanyabiashara na watendaji waandamizi wa Serikali, ulifanyika jana Ikulu, Dar es Salaam ni wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) ambalo Mwenyekiti wake ni Rais Magufuli.

Rais John Magufuli aliulizia uwepo wa mawaziri hao kwa Waziri Mkuu, Kassim majaliwa ambaye hakuwa na taarifa za kutokuwepo kwao ingawa aliwapa mwaliko wa kuwataka kuhudhuria kwani wao ni wajumbe wa mkutano huo. Hata hivyo mawaziri hao hawakutuma wawikilishi wao kwenye mkutano huo muhimu.

Kutokuhudhuria kuligunduliwa na Rais Magufuli baada ya kumtaka waziri Mpina ajibu masuala mbalimbali yaliyoibuliwa na Fuad Abri, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Asas Dairies ya Iringa kuhusu bidhaa za maziwa.

Mpina hakuwepo yeye wala mwakilishi kutoka katika wizara yake, baadaye Rais Magufuli alimtaka Waziri wa Kilimo, Tizeba aliyekuwa waziri wa wizara hiyo kabla hajaigawa lakini naye hakuwepo.

Waziri Majaliwa alisema kuwa Mawaziri wote wanaoguswa na sekta za uwekazaji hasa kwenye kilimo na mifugo hivyo walikuwa wanapaswa kuwepo kwenye mkutano huo.

Rais Magufuli alisema inasikitisha kuona baadhi ya watu aliowateua hawajaelewa anataka nini. Alisema inashangaza kuona wafanyabiashara kutoka sehemu mbalimbali nchini wamekutana na Serikali kuzungumzia masuala ya kilimo na mifugo, lakini mawaziri wa sekta hizo hawapo.

Alipotafutwa kuzungumzia kutokuwapo kwake katika mkutano huo, Mpina alisema hawezi kuzungumzia jambo hilo, bali anafuatilia kwa ukaribu kujua nini kimetokea katika mawasiliano hayo.

Ni Wazi Rais Magufuli anayeipigania Tanzania ya Viwanda kwa kuboresha sekta na mazingira rafiki kwa wawekezaji hususani katika eneo la biashara, kilimo na ufugaji hataweza kuvumilia kitendo hiki kinachodhihirisha nia mbaya kwa mazingira ya ukuaji viwanda nchini.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega alikuwa safarini mkoani Kigoma kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mifugo, Uvuvi na Maji. Na katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk. Yohana Budeba alisema yupo kikazi mjini Dodoma

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!