Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mawakili wamtosa Lissu Dar
Habari MchanganyikoTangulizi

Mawakili wamtosa Lissu Dar

Spread the love

SAKATA la Mawakili binafsi kutakiwa kugoma kufanya kazi leo limetibuka baada ya kubainika baada ya baadhi yao wamekaidi agizo la Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Tundu Lissu la kuwataka wanasheria hao kugoma, anaandika Mwandishi wetu.

Mwishoni mwa  wiki Lissu aliwataka Mawakili kugoma kufanya kazi zao kama namna ya kupinga tukio la ulipuliwaji wa Ofisi ya Mawakili wa IMMMA ya jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, MwanaHALISI Online leo imeshuhudia Mawakili hao wakiendelea na kazi zao kama kawaida katika mahakama mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Wakili Alibart Msando amesema ameshindwa kugoma kwa kuwa leo tayari alikuwa amechukua kazi za watu ambao wamemlipa fedha.

” Kuna kesi ambazo huwezi kuziepuka kuna watu wana kesi  muhimu na wengine wana mali zao wanataka ziuzwe na kama nisingetokea kesi ingeweza kufutwa,” amesema

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!