MATUKIO ya mauaji yanayotokana na wivu wa mapenzi, yameongoza katika mwaka 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar Es Salaam…(endelea).
Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 21 Desemba 2020 na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Liberatus Sabas wakati akieleza hali ya usalama nchini.
Bila kutaja idadi ya vifo hivyo, Kamanda Sabas amesema, chanzo chake ni mmomonyoko wa maadili, na kuwaomba viongozi wadini na Watanzania kwa ujumla waingilie kati kupunguza vifo hivyo.
“Haya ni mauaji ambayo yana hitaji sana kutoa elimu lakini pia kushirikisha wadau wengine wakiwemo viongozi wa dini. Mfano matukio ya mauaji kutokana na wivu wa mapenzi ambaypo kwa sas ndio yanaongoza.
Viongozi wa dini tuna amini watatoa mchango mkubwa sana, sababu yanatokana na mmomonyoko wa maadili,”amesemaKamanda Sabas.
Licha ya matukio yanayotokana na wivu wa mapenzi, Kamanda Sabas amesema vifo vingine vimetokana na imani za kishirikina na baadhi ya wananchi kujichukulia sheria mkononi.
“Matukio mengi ya mauji yana tokana na imani za kishirikiana, vifo vya mapenzi lakini pia wananchi kujichukulia sheria mkononi,” amesema Kamanda Sabas.
Aidha, Kamanda Sabas amesema matukio ya mauaji kwa kutumia silaha katika mwaka 2020 yalidhibitiwa.
“Matukio ya mauaji kwa kutumia silaha yamedhibitiwa kwa kiwango kikubwa, pia hata matukio ya mauaji kutokana na uhalifu mwingine yamepungua kwa kiasi kikubwa,” amesema Kamanda Sabas.
Leave a comment