Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mauaji wivu wa mapenzi yatikisa 2020
Habari Mchanganyiko

Mauaji wivu wa mapenzi yatikisa 2020

CP Liberatus Sabas, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Polisi
Spread the love

MATUKIO ya mauaji yanayotokana na wivu wa mapenzi, yameongoza katika mwaka 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar Es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 21 Desemba 2020 na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Liberatus Sabas wakati akieleza hali ya usalama nchini.

Bila kutaja idadi ya vifo hivyo, Kamanda Sabas amesema, chanzo chake ni mmomonyoko wa maadili, na kuwaomba viongozi wadini na Watanzania kwa ujumla waingilie kati kupunguza vifo hivyo.

“Haya ni mauaji ambayo yana hitaji sana kutoa elimu lakini pia kushirikisha wadau wengine wakiwemo viongozi wa dini. Mfano matukio ya mauaji kutokana na wivu wa mapenzi ambaypo kwa sas ndio yanaongoza.

Viongozi wa dini tuna amini watatoa mchango mkubwa sana, sababu yanatokana na mmomonyoko wa maadili,”amesemaKamanda Sabas.

Licha ya matukio yanayotokana na wivu wa mapenzi, Kamanda Sabas amesema vifo vingine vimetokana na imani za kishirikina na baadhi ya wananchi kujichukulia sheria mkononi.

“Matukio mengi ya mauji yana tokana na  imani za kishirikiana, vifo vya mapenzi lakini pia wananchi kujichukulia sheria mkononi,” amesema Kamanda Sabas.

Aidha, Kamanda Sabas amesema matukio ya mauaji kwa kutumia silaha katika mwaka 2020 yalidhibitiwa.

“Matukio ya mauaji kwa kutumia silaha yamedhibitiwa kwa kiwango kikubwa, pia hata matukio ya mauaji kutokana na uhalifu mwingine yamepungua kwa kiasi kikubwa,” amesema Kamanda Sabas.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!