WATAHINIWA 733,103 kati ya 943,318 wamefaulu mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi wa mwaka 2018. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Akitangaza matokeo hayo leo tarehe 23 Oktoba 2018 jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde amesema ufaulu huo ni ongezeko la asilimia 4.96 kutoka asimilia 72.76 kwa mwaka jana hadi kufikia 77.725 mwaka 2018.
Dk. Msonde amesema takwimu zinaonyesha kuwa ufaulu katika masomo ya Maarifa ya Jamii, Kiingereza, Sayansi na Hisabati umepanda kwa asilimia kati ya 4.03 na 11.92 wakati somo la Kiswahili ukishuka kwa asilimia 1.44 ikilinganishwa na ufaulu ulivyokuwa mwaka 2017.
Katika hatua nyingine, Dk. Msonde amesema kati ya wanafunzi waliofaulu mtihani huo, wasichana walikuwa 383,830 idadi ambayo ni sawa na asilimia 77.12 na wavulana 350,273 (78.38)
Leave a comment