Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Masikini Wema! Atupwa mahabusu
Habari MchanganyikoMichezo

Masikini Wema! Atupwa mahabusu

Wema Sepetu (mwenye gauni jeusi) akitolewa mahakamani na kupelekwa mahabusu
Spread the love

WEMA Sepetu, mwigizaji na msanii maarufu wa filamu nchini, amejisalimisha na kutupwa mahabusu baada ya Mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam kuagiza kusakwa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Maira Kasonde, Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo tarehe 11 Juni 2019, alitoa amri ya kumkamata Wema popote alipo baada ya kushindwa kufika mahakamani ili kusikiliza kesi yake inayohusu kuchapisha video chafu mtandaoni.

Msanii huyo amekamatwa leo tarehe 17 Juni 2019, katika Mahakama ya Kisutu baada ya mahakama hiyo kutoa wito wa kukamatwa kwake.

Alipofika mahakamani, Wema alikamatwa na kupandishwa kwenye gari la Magereza na kupelekwa Segerea. Anatarajiwa kufikishwa mahakamani hapo tarehe 24 Juni 2019. Siku hiyo mahakama itaamua kumfutia dhamana ama la!

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!