Thursday , 25 April 2024
Habari za Siasa

Masikini Abdul Nondo!

Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT-Wazalendo
Spread the love

MAHAKAMA ya Mkoa wa Iringa imemkuta na kesi ya kujibu Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini (TSNP) Abdul Nondo aliyeshitakiwa kwa madai ya kusambaza taarifa za uongo kwamba ametekwa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Leo tarehe 27 Agosti 2018, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Liad Chamshama ametoa uamuzi huo kutokana na ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo na upande wa Jamhuri. Hakimu amemtaka Nondo andae utetezi wake.

Hakimu Chamshama amesema kuwa, kutokana na ushahidi uliowasilishwa na upande wa Jamhuri mahakama hiyo imemtaka Nondo kujibu tuhuma hizo.

Nondo ameshitakiwa mahakamani hapo kwa kosa la kusambaza taarifa za uongo kupita mtandao wa WhatsApp na kumdanganya Ofisa wa Polisi kwenye Kituo cha Polisi cha Mafinga.

Nondo alidaiwa kutenda kosa hilo tarehe 7 Machi mwaka huu akiwa eneo la Ubungo Jiji Dar es Salaam na Mafinga mkoani Iringa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!