Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Mashabiki kuandamana Messi kuondoka Barcelona
Michezo

Mashabiki kuandamana Messi kuondoka Barcelona

Spread the love

BAADA ya mshambuliaji wa klabu ya FC Barcelona, Lionel Messi kutuma maombi maalumu kwa uongozi ya kutaka kuondoka kwenye klabu hiyo, mashabiki wa klabu hiyo wameonekana kujikusanya katika mitaa mbalimbali ya kwenye kitongoji cha Catalunya kuonesha kutokubaliana na jambo hilo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Jana jumanne 25 Agosti, 2020 mshambuliaji huyo alituma maombi maalumu ya kuondoka kwenye klabu ambayo ameitumikia kwenye maisha yake yote kwenye mchezo wake wa soka.

Taarifa kutoka katika vyanzo mbalimbali zinaeleza kuwa bodi ya klabu hiyo huwenda ikakutana hivi karibuni na pengine Rais wa klabu hiyo Josep Maria Bartomeu’s akajiuzuru kutokana na kuonekana ndiyo sababu kubwa ya mchezaji huyo kuchukua maamuzi hayo.

Kilichopo kwa sasa kati ya Messi na jopo lake pamoja na klabu ya Barcelona ni kuwekana sawa katika vipengele cha mkataba, ambapo moja ya kipengele kwenye mkataba wake ni endapo kama kuna klabu yoyote itamtaka huduma ya mchezaji huyo itoe kiasi cha Tsh. 1.9 trilioni.

Lionel Messi

Messi amechukua maamuzi hayo baada ya kupoteza kwenye mchezo wa nusu fainali ya Klabu Bingwa Ulaya kwa mabao 8-2 dhidi ya klabu ya FC Bayern kutoka Ujerumani na uongozi kuamua kumtimua kocha wao Quique Setien.

Tayari klabu hiyo imeshamtangaza, Ronald Koeman kuja kuchukua mikoba ya Setien licha ya Messi kukataa kufanya mazungmzo naye na kumueleza kuwa anataka kuhama kwenye klabu hiyo.

Lakini pia ameonekana kutokuwa na furaha kutokana na jinsi kocha huyo mpya alivyosema kuwa hana mpango wa kumtumia Luis Suarez ambaye ni swahiba mkubwa wa Lionel Messi.

Mashabiki wengi wa klabu hiyo wameonekana kutokukubaliana na swala hilo na kumtaka Rais wa klabu hiyo Bartomeus kuachia ngazi mara moja ili kumnusuru mshambuliaji huyo kuondoka kwenye klabu hiyo.

Messi mwenye umri wa miaka 33 alijiunga katika shule ya kukuza vipaji ya Barcelona toka 2001, na kuitumikia klabu hiyo kwa mafanikio makubwa huku akishinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia ‘Ballon D’or’ mara sita akiwa mbele ya Cristiano Ronaldo alitwaa tuzo hiyo mara tano.

Aidha Messi amefanikiwa kutwaa taji la Ligi Kuu nchini Hispania mara 10, klabu bingwa Ulaya mara nne, kombe la Ligi mara sita, klabu bingwa dunia mara tatu na tuzo ya mchezaji bora wa Ligi kuu nchini mara nane.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!