MAREKANI imeitaka serikali ya Rais wa Uganda, Yoweri Museveni kufuta mashtaka ya uhaini iliyofungua mahakamani dhidi ya Mbunge wa Kyadondo Mashariki , Robert Kyagulanyi ‘Bobi Wine’ na wenzake. Anaripoti Regina Kelvin…(endelea).
Baraza la Wawakilishi la Marekani, limetoa wito huo kupitia barua yake iliyowasilisha hivi karibuni kwa Balozi wa Uganda nchini humo, Mull Katende ikidai kuwa mashtaka dhidi ya Bobi Wine na wenzake 32 yalikuwa yakupangwa.
Vile vile, Marekani imetoa wito kwa serikali ya Uganda kufanya uchunguzi huru ili kubaini aliyehusika katika vurugu zilizotokea mjini Arua nchini humo, ambapo inadaiwa kwenye vurugu hizo msafara wa Rais Museveni ulirushiwa mawe.
Katika hatua nyingine, baraza hilo limesema limesikitishwa na baadhi ya maafisa wa vyombo vya dola kutumia nguvu dhidi ya raia hasa wafuasi wa upinzani nchini Uganda.
Leave a comment