Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani yaikomalia Afghanistan, yasitisha misaada
Kimataifa

Marekani yaikomalia Afghanistan, yasitisha misaada

Donald Trump
Spread the love

MISAADA  ya kiusalama kwa Pakistan yenye thamani ya takriban dola milioni 900 itasitishwa hadi pale Pakistan itakapochukua hatua madhubuti ya kupambana na kundi la wanamgambo wa Afghanistan la Taliban na la Haqqani.

Hatua hiyo ilitangazwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani huku ikisema Rais Donald Trump amekerwa na  Pakistan kushindwa kuchukua hatua za kutosha dhidi ya makundi hayo mawili ambayo yamekuwa yakiitumia nchi hiyo kama sehemu ya kujificha na kufanya mashambulizi katika nchi jirani ya Afghanistan.

Ufadhili huo utakaositishwa utaathiri ununuzi wa vifaa vya kijeshi, mafunzo, huduma nyingine za kijeshi na mpango wa kupambana na ugaidi.

Akiwahutubia wanahabari, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Marekani,  Heather Nauert amesema hatua hiyo ya kusitisha ufadhili, haitaathiri misaada inayotolewa kwa raia wala ile ya kusaidiai uchumi wa Pakistan.

Nauert amesema fedha hizo huenda zikaidhinishwa kutolewa iwapo Pakistan itachukua hatua zinazostahili kukabiliana na makundi ya kigaidi.

Bunge la Marekani limefahamishwa kuhusu uamuzi huo wa kustishia misaada kwa Pakistan.

Pakistan kwa muda mrefu imekanusha shutuma kuwa imeshindwa kupambanana na makundi ya wanamgambo yanayopambana dhidii ya majeshi ya Afghanistan na ya kigeni kutokea upande wa pili wa mpaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!