Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani, Kenya wasaini mkataba wa usalama, biashara
Kimataifa

Marekani, Kenya wasaini mkataba wa usalama, biashara

Spread the love

DONALD Trump, Rais wa Marekani na Rais Uhuru Kenyetta wa Kenya wamesaini mikataba yenye thamani ya dola za kimarekani 900 milioni, huku sehemu kubwa ya makubaliano ya mikataba hiyo ikiwa ni masuala ya usalama na biashara. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Trump na Kenyatta wamesaini mikataba hiyo jana tarehe 27 Agosti, 2018 walipokutana kwa ajili ya kufanya mazungumzo kwenye Ikulu ya ‘White House’ iliyoko mjini Washington nchini Marekani.

Marais hao  kwa pamoja walikubaliana kushirikiana katika kupambana na masuala ya usalama na ulinzi hasa kudhibiti vitendo vya kigaidi pamoja na kuboresha ushirikiano katika biashara na uwekezaji.

Katika hatua nyingine, viongozi hao wakuu wa nchi walijadiliana kuhusu masuala ya usafiri, ikiwemo  safari za moja kwa moja kutoka Nairobi nchini Kenya hadi New York nchini Marekani zitakazo anza mwezi Oktoba, 2018 na kuweka mikakati ya kuhakikisha kwamba safari hizo zitaimarisha utalii na biashara kwa manufaa ya nchi hizo mbili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!