Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marais wastaafu Marekani wamsulubu Trump
Kimataifa

Marais wastaafu Marekani wamsulubu Trump

Donald Trump, Rais wa Marekani
Spread the love

MARAIS wastaafu wa Marekani, Bill Clinton na Jimmy Carter wamesema Donald Trump, rais wa sasa wa Taifa hilo amesababisa vurugu kwa taifa hilo. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Wametoa kauli hiyo baada ya Joel Biden kuidhinishwa rasmi na Chama cha Democratic kuwania urais kupitia chama hicho, kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Novemba 2020.

Clinton aliyeongoza Marekani kuanzia 1993-2001, kwenye hotuba yake usiku wa kuamkia leo Jumatano tarehe 19 Agosti 2020, amesema Marekani ndio nchi iliyopiga hatua kubwa kiuchumi duniani lakini watu waliokosa ajira wameongezeka mara tatu zaidi katika uongozi wa Trump.

Amesema, utawala wa Trump umeshindwa kutatua changamoto ya ajira pamoja na tatizo la janga la corona kutokana na mbinu zisizokuwa na makali kutumika.

Carter aliyeongoza taifa hilo kuanzia Januari 1977 – Januari 1981 ameeleza kushangazwa na Trump katika kukabiliana na mihemuko ya Wamarekani huku akigusia uhusiano wa Marekani na nchi za nchi ulivyoyumba.

Wastaafu wote kwa pamoja, wameeleza kumuunga mkono Biden kutokana na kile walichoita historia yake na uwajibikaji wake katika maeneo mbalimbali aliyopita.

Carter amewataka Wamarekani kutofanya kosa, kwa kuwa nafasi ya kufanya marekebisho imebaki moja nayo ni kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Colin Powell, Waziri wa Wambo ya Nje mstaafu na mwanachama wa Chama cha Republican amemtaja Biden kwamba, ni mtu mwenye maadili aliyojifunza wakati mwanajeshi na kwamba anamuunga mkono ili arejeshe maadili katika Ikulu ya nchi hiyo.

Powell, aliyehudumu nafasi hiyo wakati wa utawala wa Rais George W. Bush, anamtaja Trump kama kiongozi muongo.

Waziri huyo mstaafu anaungana na wanachama wengine wa Republican ambao wameridhishwa na uamuzi wa Democratic kumuidhinisha Biden kuwa mgombea urais.

Mwanachama mwingine maarufu wa Republican anayemuunga mkono mgombea wa Democratic ni aliyekuwa gavana wa Ohio, John Kasich.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!