Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Maofisa 4 NEMC mbaroni tuhuma za utakatishaji fedha
Habari Mchanganyiko

Maofisa 4 NEMC mbaroni tuhuma za utakatishaji fedha

Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), inawashikilia watumishi wanne wa Baraza la Taifa la Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo makosa ya rushwa na utakatishaji fedha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Watuhumiwa hao, wanashikiliwa katika ofisi za Takukuru, Upanga jijini Dar es Salam na kesho Alhamisi tarehe 4 Juni 2020 watafikishwa mahakamani.

Taarifa ya Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani aliyoitoa leo Jumatano tarehe 3 Juni 2020 imesema, watuhumiwa hao wamekuwa wakichunguzwa kwa makosa mbalimbali na uchunguzi huo umekamilika.

Amewataja watuhumiwa hao ni; Deusdedith Katwale, Magori Matiku na Obadia Machupa ambao wote ni maafisa mazingira na Lydia Nyinondi ambaye ni Mhasibu Msaidizi. Wote wa makao makuu.

Doreen ametaja tuhuma zao ni; kula njama na kutenda kosa, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo, kuisababishia mamlaka hasara, matumizi mabaya ya madaraka pamoja na utakatishaji wa fedha haramu.

“Tunapenda kuujulisha umma pia, Takukuru kwa kushirikiana na ofisi ya taifa ya mashtaka inatarajia kuwafilisha watuhumiwa hawa mahakamani kesho tarehe 4 Juni 2020,” amesema Doreen

Katikati hatua nyingine, Doreen amesema, Takukuru inamshikilia Eliud Kijalo ambaye ni Afisa wa wizara ya maliasili na utalii kwa makosa ya ubadhirifu wa zaidi ya Sh. 4 bilioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!