YUSUF Manji, anayejitambua kama Mwenyekiti wa Yanga, anatarajia kuongoa Mkutano Mkuu wa dharura wa klabu hiyo unaotarajia kufanyika kesho, ambao mpaka sasa haujafahamika utafanyika wapi wala ajenda za mkutano huo hazijajulikana. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Akiongea na moja ya kituo cha radio leo asubuhi Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya klabu hiyo, Hussein Nyika amesema kuwa bado wanatafuta ukumbi ambao utaweza kutosha wanachama wote watakaohudhuria mkutano huo siku ya kesho ambao utakaoongozwa na Manji.
“Mkutano kesho upo palepale ila kwa sasa tunatafuta ukumbi utakaoweza kutosha kufanyikia mkutano huo, ambao utaongoza na Yusuph Manji ambao bado sisi tunamtambua kama Mwenyekiti wa Yanga na wanachama kufanya maamuzi,” amesema Nyika.
Hivi karibuni Manji aliandika barua ya kukubali ombi la wanachama kurudi katika nafasi yake kama Mwenyekiti ndani ya klabu hiyo kutokana na mapendekezo ya mkutano mkuu uliofanyika 10 Juni, 2018, na barua yake iliwasilishwa na Mwenyekiti wa baraza la Wadhamini, Kapteni George Mkuchika mbele ya wana habari.
Mkutano huo ambao unaenda kufanyika huku mchakato wa uchaguzi wa kujaza nafasi zilizoachwa wazi ukitarajia kufanyika 13 Januari, 2019, katika nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wanne wa kamati ya utendaji.
Leave a comment