Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Manji kuongoza Mkutano Mkuu Yanga kesho
Michezo

Manji kuongoza Mkutano Mkuu Yanga kesho

Yusuf Manji
Spread the love

YUSUF Manji, anayejitambua kama Mwenyekiti wa Yanga, anatarajia kuongoa Mkutano Mkuu wa dharura wa klabu hiyo unaotarajia kufanyika kesho, ambao mpaka sasa haujafahamika utafanyika wapi wala ajenda za mkutano huo hazijajulikana. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Akiongea na moja ya kituo cha radio leo asubuhi Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya klabu hiyo, Hussein Nyika amesema kuwa bado wanatafuta ukumbi ambao utaweza kutosha wanachama wote watakaohudhuria mkutano huo siku ya kesho ambao utakaoongozwa na Manji.

“Mkutano kesho upo palepale ila kwa sasa tunatafuta ukumbi utakaoweza kutosha kufanyikia mkutano huo, ambao utaongoza na Yusuph Manji ambao bado sisi tunamtambua kama Mwenyekiti wa Yanga na wanachama kufanya maamuzi,” amesema Nyika.

Hivi karibuni Manji aliandika barua ya kukubali ombi la wanachama kurudi katika nafasi yake kama Mwenyekiti ndani ya klabu hiyo kutokana na mapendekezo ya mkutano mkuu uliofanyika 10 Juni, 2018, na barua yake iliwasilishwa na Mwenyekiti wa baraza la Wadhamini, Kapteni George Mkuchika mbele ya wana habari.

Mkutano huo ambao unaenda kufanyika huku mchakato wa uchaguzi wa kujaza nafasi zilizoachwa wazi ukitarajia kufanyika 13 Januari, 2019, katika nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wanne wa kamati ya utendaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!