Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mange Kimambi ‘shujaa’ Afrika
Habari MchanganyikoTangulizi

Mange Kimambi ‘shujaa’ Afrika

Mange Kimambi siku aliyofanya maandamano ya kupinga vitendo vinavyofanywa kinyume na haki za binadamu
Spread the love

TUZO ya mwanamke mwenye ushawishi na mhamasishaji zaidi kisiasa Afrika imechukuliwa na Mange Kimambi, raia wa Tanzania. Anaripoti Regina Kelivin … (endelea).

Waandiaaji wa tuzo hiyo wanaotambulika kwa jina la kingereza Black Entertainment Film Fashion Television and Art (BEFFTA) –Burudani, Filamu, Mitindo, Televisheni ya Watu Aweusi wamemchagua Mange kuwa mshindi wa tuzo hiyo dhidi ya wenzake.

Waliokuwa kwenye kinyang’anyiro hicho ni pamoja ni Elie Johson Sirleaf wa Liberia, Joice Majuru kutoka Zimbabwe, Diane Shima Rwigara raia wa Rwanda, Mbali Ntuli kutoka Afrika Kusini na Alengot Oromait kutoka nchini Uganda.

Lengo la BEFFTA ni kuangaza maslahi ya watu weusi katika nchi za Uingereza, Canada, Marekani, Carribbean na nchi za Bara la Afrika.

Awali taarifa za kuwania tuzo hizo zilitolewa na shirika hilo la BFFTA kupitia ukurasa wao unaopatikana kwenye mtandao wa kijamii wa instagram.

Mange amejipatia umaarufu katika mitandao ya kijamii hasa instagram kutokana jumbe zake za ukosoaji kwa viongozi wa serikali na hata viongozi wa dini nchini Tanzania.

Pia aliongeza ‘presha’ zaidi Tanzania kutokana na kutumia mitandao ya kijamii kuhamasisha maandamano aliyopanga kufanyika Aprili 26 mwaka huu.

Hatua hiyo hiyo iliwalazimu viongozi mbalimbali Tanzania kujitokeza na kupinga maandamano hayo yaliyoonekana kushika kasi kupitia mitandao hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!