BAADA ya kusimama kwa takriban miezi mitatu, hatimaye Ligi Kuu nchini England kurejea kesho kwa michezo miwili ambapo klabu ya Manchester City itaikalibisha Arsenal kwenye uwanja wa Etihad. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Mchezo huo ambao ulikuwa wa kiporo wa mzunguko wa pili utazikutanisha klabu hizo ambazo zina historia kubwa kesho soka la England ambapo mchezo wa mwisho Arsenal alipoteza kwa mabao 3-0, kwenye uwanja wa Emirates.
Ligi hiyo ambayo imebakiza michezo tisa kumalizika inarejea baada ya mlipuko wa ugonjwa wa Covid 19 uliosababisha kusimamishwa na chama cha soka nchini humo (FA) huku klabu ya Liverpool ikiwa kinara kwenye msimamo baada ya kujikusanyia pointi 82.
Mchezo mwingine siku ya kesho utaikutanisha klabu ya Astorn Villa anayochezea mtanzania Mbwana Samatta dhidi ya Sheffield United na siku ya Ijumaa, Manchester United itashuka dimbani kuikabili Tottenham, Norwich city dhidi ya Southampton.
Leave a comment