JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema linamshikilia Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo kwa kosa la kutoa taarifa za uongo na kujiteka. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Kanda ya Dar es Salaam, amewaaambia waandishi wa habari leo, Nondo ambaye pia ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam atafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika.
Mambosasa amesema Nondo alidaiwa kutoweka jijini Dar es Salaam Machi 6, 2018, lakini alionekana wilayani Mafinga siku inayofuata na kujisalimisha mikononi mwa polisi Machi 7 mwaka huu.
Kamanda huyo amesema baada ya kujisalimisha alifunguliwa jalada la uchunguzi na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire, wanaendelea kumchunguze kubaini iwapo ni kweli alitekwa au alitoa taarifa za uongo kwa lengo la kuhamasisha wanafunzi kuvuruga amani.
Leave a comment