Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mambosasa: Tunamshikilia Nondo kwa kutoa taarifa ya uongo
Habari za SiasaTangulizi

Mambosasa: Tunamshikilia Nondo kwa kutoa taarifa ya uongo

Mkurugenzi wa Idara ya Haki na Wajibu wa Wanafunzi Tanzania, Abdul Nondo
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema linamshikilia Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo kwa kosa la kutoa taarifa za uongo na kujiteka. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Kanda ya Dar es Salaam, amewaaambia waandishi wa habari leo, Nondo ambaye pia ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam atafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika.

Mambosasa amesema Nondo alidaiwa kutoweka jijini Dar es Salaam Machi 6, 2018, lakini alionekana wilayani Mafinga siku inayofuata na kujisalimisha mikononi mwa polisi Machi 7 mwaka huu.

Kamanda huyo amesema baada ya kujisalimisha alifunguliwa jalada la uchunguzi na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire, wanaendelea kumchunguze kubaini iwapo ni kweli alitekwa au alitoa taarifa za uongo kwa lengo la kuhamasisha wanafunzi kuvuruga amani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!