Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mambo yatakayofanywa na SADC chini ya Rais Magufuli
Habari za Siasa

Mambo yatakayofanywa na SADC chini ya Rais Magufuli

Rais John Magufuli, Mwenyekiti wa Jumuiya ya SADC akihutubia wajumbe wa mkutano huo
Spread the love

JANA tarehe 18 Agosti 2019 Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi 16 mwanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ulifungwa rasmi, huku wajumbe walioshiriki mkutano huo wakipitisha maazimio kadhaa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mkutano wa 39 wa SADC ulifanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 17 hadi 18 Agosti mwaka huu, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere  (JNIC) jijini Dar es Salaam.

Siku ya kwanza ya mkutano huo, Rais Magufuli alikabidhiwa uenyekiti wa SADC na mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Dk. Hage Geingob ambaye ni Rais wa Namibia. Pia, siku hiyo lugha ya Kiswahili ilitangazwa kuwa miongoni mwa lugha nne rasmi za jumuiya hiyo.

Rais John Magufuli ametaja maazimio yaliyofikiwa na wakuu hao wa nchi, ambayo yatatekelezwa wakati akiwa Mwenyekiti wa SADC.

Miongoni mwa maazimio hayo, ni nchi mwanachama wa jumuiya hiyo kuendelea na utekelezaji wa mkakati na mwongozo wa maendeleo ya viwanda wa SADC wa mwaka 2015 hadi 2063.

Pia, wajumbe wa SADC waliazimia kuendelea na uwekezaji katika sekta ya miundombinu, kwa ajili ya kuchochea ukuaji wa uchumi pamoja na kuboresha sera za uchumi na fedha za jumuiya hiyo.

Azimio lingine alilotaja Rais Magufuli, ni nchi mwanachama wa SADC kuendelea kufuatilia hali ya usalama katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), pamoja na sekretarieti ya jumuiya hiyo kuanzisha chombo cha kukabiliana na majanga.

Licha ya maazimio hayo, wajumbe wa SADC walijadili maombi ya nchi ya Burundi kujiunga na SADC na kuitaka sekretarieti ya jumuiya hiyo kuitaarifu serikali ya Burundi taratibu ambazo inatakiwa kukamilisha ili ombi lake la kujiunga liweze kukubaliwa.

Vile vile, Rais Magufuli amesema wajumbe wa SADC wamekubaliana kuendelea kuwasiliana na Jumuiya za Kimataifa ili iiondolee vikwazo nchi ya Zimbabwe.

Katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wa Rais Magufuli SADC, nchi nne za jumuiya hiyo zinatarajia kufanya uchaguzi ambazo ni Malawi, Botswana, Mauritius na Msumbiji, ambapo amezitakia kheri nchi hizo ili zitekeleze zoezi hilo kwa amani na utulivu.

Rais Magufuli atakuwa mwenyekiti wa SADC katika kipindi cha mwaka mmoja kuanzia mwezi Agosti mwaka huu mpaka Agosti 2020 ambapo anatarajiwa kukabidhi kijiti hicho kwa Rais wa Msumbiji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!