Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mama Samia: Watanzania ni hodari kutengeneza sera, si kuzitumia
Habari za Siasa

Mama Samia: Watanzania ni hodari kutengeneza sera, si kuzitumia

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hasani amesema, Watanzania ni mahodari kutengeneza sera, sheria na kanuni lakini siyo watekelezaji. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Ametoa kauli hiyo leo 31 Julai 2019 kwenye kongamano la ufunguzi wa jukwaa kuhusu ‘usimamizi bora wa misitu kwa upatikanaji wa rasilimali maji endelevu”’iliyofanyika jijini Dodoma chini ya Taasisi ya Uongozi.

Katika kongamano hilo Mama Samia amesema, Tanzania imekuwa na wataalamu wengi wenye kujua kuelezea mipango, sara, kanuni na sheria viziri katika makongamano ya kitaifa hivyo kupewa pesa za utunzaji, lakini utekelezaji duni.

Kutokana na hali hiyo amesema, umefika wakati wa kufanya kazi kwa vitendo na siyo kukaa ofisini na vikao kwa lengo la kuhesabiana posho.

Mbali na hilo amesema, takwimu za mwaka 2015 zilizotolewa na Maliasili na Utalii zinaonesha, Tanzania imepoteza heka 372,816.

Na kuwa, uharibifu huo unatokana na shughuli za kibinadamu kuwa nyingi hasa katika misitu isiyokuwa na usimamizi wa kisheria.

Amesema, takwimu zilizotolewa na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine mkoani Morogoro mwaka 2017, kiwango cha kutoweka misitu kimefikia hekta 469,420 kwa mwaka.

“Hili ni sawa na ongezeko la hekta takribani 100,000 ndani ya miaka miwili, hali hii siyo rafiki kwa upatikanaji endelevu wa rasilimali maji,” amesema.

Amesema, kukosekana kwa misitu kunasababisa kuchelewa kwa maendeleo ya nchi.

Akizungumzia uharibifu wa mazingira amesema, hakuna siku ambayo moyo wake uliumia alipoona wanyama wakipanga foleni kunywa maji.

“Kuna siku niliumia sana maana niliona jambo la ajabu ambalo sijawabi kuliona duniani. Jambo hilo ni pale nilipokuwa Ruaha na kuona wanyama wakipanga foleni kunywa maji huku wakimtegemea  Tempo awe ndiye anayechimba shimo maji yatoke ili wayapate,” amesema Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!