MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hasani amesema, Watanzania ni mahodari kutengeneza sera, sheria na kanuni lakini siyo watekelezaji. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).
Ametoa kauli hiyo leo 31 Julai 2019 kwenye kongamano la ufunguzi wa jukwaa kuhusu ‘usimamizi bora wa misitu kwa upatikanaji wa rasilimali maji endelevu”’iliyofanyika jijini Dodoma chini ya Taasisi ya Uongozi.
Katika kongamano hilo Mama Samia amesema, Tanzania imekuwa na wataalamu wengi wenye kujua kuelezea mipango, sara, kanuni na sheria viziri katika makongamano ya kitaifa hivyo kupewa pesa za utunzaji, lakini utekelezaji duni.
Kutokana na hali hiyo amesema, umefika wakati wa kufanya kazi kwa vitendo na siyo kukaa ofisini na vikao kwa lengo la kuhesabiana posho.
Mbali na hilo amesema, takwimu za mwaka 2015 zilizotolewa na Maliasili na Utalii zinaonesha, Tanzania imepoteza heka 372,816.
Na kuwa, uharibifu huo unatokana na shughuli za kibinadamu kuwa nyingi hasa katika misitu isiyokuwa na usimamizi wa kisheria.
Amesema, takwimu zilizotolewa na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine mkoani Morogoro mwaka 2017, kiwango cha kutoweka misitu kimefikia hekta 469,420 kwa mwaka.
“Hili ni sawa na ongezeko la hekta takribani 100,000 ndani ya miaka miwili, hali hii siyo rafiki kwa upatikanaji endelevu wa rasilimali maji,” amesema.
Amesema, kukosekana kwa misitu kunasababisa kuchelewa kwa maendeleo ya nchi.
Akizungumzia uharibifu wa mazingira amesema, hakuna siku ambayo moyo wake uliumia alipoona wanyama wakipanga foleni kunywa maji.
“Kuna siku niliumia sana maana niliona jambo la ajabu ambalo sijawabi kuliona duniani. Jambo hilo ni pale nilipokuwa Ruaha na kuona wanyama wakipanga foleni kunywa maji huku wakimtegemea Tempo awe ndiye anayechimba shimo maji yatoke ili wayapate,” amesema Samia.
Leave a comment