Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makontena ya Makonda kupigwa mnada J’mosi
Habari za Siasa

Makontena ya Makonda kupigwa mnada J’mosi

Spread the love

BAADA ya mnada wa kwanza wa makontena 20 yenye samani yaliyoingizwa na Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kukwama, Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imepanga kufanya mnada wa pili Jumamosi ya Septemba mosi, 2018. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

TRA imetaarifu kuwa, imedhamiri kurudia mnada huo wa makontena yenye samani za ofisi ikiwemo meza na viti, ambayo yamekwama katika bandari kavu ya Dar es Salaam kutokana na kudaiwa kodi ya kaisi cha Sh. 1.2 bilioni.

Mamlaka hiyo imetoa wito kwa wananchi kujitokeza katika mnada huo kununua samani hizo kwa kufuata taratibu na sheria za minada.

Aidha, TRA imewatoa hofu wananchi kuhusu kauli iliyotolewa na Makonda ya kwamba atakaye nunua makontena hayo atalaaniwa na Mungu.

Baada ya mnada wa kwanza uliofanyika tarehe 25 Agosti, 2018 kukwama kutokana na wateja kushindwa kufika bei elekezi, Makonda alitoa kauli akisema kuwa, mtu atakayenunua makontena hayo atapata laana kwa kuwa, makontena hayo yenye samani yaliingizwa nchini kwa ajili ya kuwasaidia waalimu wa mkoa wa Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!