Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Makonda: Serikali imetenga Bil 200 ujenzi miundombinu
Habari Mchanganyiko

Makonda: Serikali imetenga Bil 200 ujenzi miundombinu

Mafuriko Jangwani
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania, imetenga jumla ya shilingi 200 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu kuzunguka Mto Msimbazi, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam leo tarehe 14 Mei 2019, katika eneo la Jangwani ikiwa ni siku moja baada ya maji kufurika eneo hilo.

Maji hayo yalifurika Jangwani na kusababisha mafuriko huku miundombinu ikiharibiwa ikiwa ni pamoja na magari kuzuiwa kupita.

“Kutokana na adha ambayo imeendelea kujitokeza katika eneo la Jangwani, serikali imetafuta fedha kupitia Benki ya Dunia na pesa iliyotengwa ni zaidi ya Dola Milioni 100.

“Hii ni zaidi ya Bilioni 200, baada ya upembuzi yakinifu kuna uwezekano pesa ikaongezeka au ikapungua kulingana na mahitaji yatakayokuwepo, matumaini yangu jambo hili litakalimika ndani ya muda mfupi,” amesema.

Katika hatua nyingine Makonda amewataka wakazi wa Dar es Salaam kuzingatia usafi, ili kuepuka magojwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.

“Ninazo taarifa kuna baadhi ya ndugu zetu wameua kurudi kwenye nyumba zao baada ya kuona maji yamekauka, lakini maji wanayotumia kupigia deki ndio hayo yaliyochanganyika na vinyesi na yaliyofunguliwa kutoka kwenye chemba ambayo yanamadhara makubwa zaidi ya kupata magonjwa ya mlipuko pamoja na kipindupindu.

“Wale tuliotoka kwenye maeneo tungesubiri ili hali iwe shwari ili turudi sehemu iliyokuwa salama zaidi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!