Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Makambo ruksa kuivaa USM Alger
Michezo

Makambo ruksa kuivaa USM Alger

Heritier Makambo
Spread the love

MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga, Heritier Makambo amepewa ruhusa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika ‘CAF’ kuitumikia klabu hiyo katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger utakaofanyika tarehe 19 Agosti, mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Hapo awali uongozi wa klabu hiyo ulipeleka majina ya wachezaji watatu kwenye shirikisho hilo ambao ni Deus Kaseke, Matheo Antony na Heritier Makambo ili kuongeza nguvu kwenye kikosi chao baada ya kufanikiwa kufuzu kwenye hatua ya makundi ya michuanio hiyo huku kanuni zikiwaruhusu kufanya hivyo.

Yanga yenye alama moja ambayo inashika nafasi ya mwisho kwenye kundi D baada ya kucheza michezo minne, huku ikipoteza michezo mitatu na kwenda sare mmoja, hivyo kupoteza matumaini ya kusonga mbele kwenye hatua ya nusu fainali ya michuani hiyo.

Katika mchezo ujao dhidi ya USM Alger utakuwa kipimo tosha kwa mshambuliaji huyo raia wa DR Congo ambaye ameingia kandarasi ya kuitumikia klabu hiyo kwa miaka miwili, huku likiwa pendekezo la kocha mkuu wa klabu hiyo Mwinyi Zahera ambaye atakiongoza kikosi hicho katika msimu ujao wa mashindano.

Katika hatua nyingine klabu hiyo inatarajia kucheza mchezo maarumu wa kirafiki kwa ajili ya kumuaga aliyekuwa nahodha wa kikosi hicho Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ambaye ametundika daruga, kwenye uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!