Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Majina waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza haya hapa
ElimuHabari Mchanganyiko

Majina waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza haya hapa

Wanafunzi wa darasa la saba wakifanya mtihani
Spread the love

BARAZA la Mitihani nchini (NECTA), limetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza nchini. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Akitangaza majina hayo leo tarehe 5 Desemba 2019, Selemani Jafo, Waziri wa Ncho, Ofisi ya Rais –Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) amesema, asilimia 92.27 ya wanafunzi waliofanya mtihani wa Darasa la Saba mwaka huu, wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza mwakani.

Amesema, asilimia hiyo inaakisi jumla ya wanafunzi 701,038 kwamba ndio waliochaguliwa.

Amesema, wanafunzi 58,699 wameshindwa kuchaguliwa kutokana na kukosa madarasa huku Mkoa wa Kigoma, ukiwa na kiwango kikubwa cha upungufu huo. Wanafunzi 909 ndio waliofutiwa matokeo kutokana na udanganyifu.

Amesema, katika wale waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza, wavulana ni 335, 513 na wasichana ni 365, 525.

Angalia majina ya wanafunzi wa darasa la saba na shule wanazoenda hapa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!