BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imetoa majina 30,675 ya wanafunzi watakaopata mikopo kwa mwaka 2019/20. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Orodha ya majina hayo imetolewa na Abdul-Razaq Badru ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa bodi, na kwamba idadi ya waombaji ilikuwa wanafunzi 45, 000.
Akitoa ufafanuzi Badru amesema, idadi hiyo ya waliopata mikopo ni ya awamu ya kwanza, mkopo ambapo jumla ya Sh. 113 Bil zitatumika kwa mikopo hiyo.
Amesema, majina ama orodha ya wanafunzi watakaopata mikopo kwa awamu ya pili, itatangazwa tarehe 25 Oktoba 2019.
Leave a comment