Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa azindua safari za treni ya mizigo Tanga-Moshi
Habari Mchanganyiko

Majaliwa azindua safari za treni ya mizigo Tanga-Moshi

Spread the love

KASSIM Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amezindua safari za treni za mizigo kutoka Mkoa wa Tanga kuelekea Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hafla ya uzinduzi huo imefanyika leo tarehe 20 Julai 2019 katika viwanja vya Stesheni ya Moshi, mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Majaliwa amesema utekelezaji wa urejeshaji huduma ya usafiri wa reli nchini, ni muendelezo wa jitihada za serikali katika kufikisha huduma muhimu kwa jamii.

Majaliwa amesema serikali itaanzisha usafiri wa treni ya abiria kutoka Dar es Salaam, Moshi hadi Arusha.

“Tunaendelea kuboresha miundombinu ya reli ili kuifungamanisha na sekta nyingine, ndiyo maana tumewekeza katika ujenzi wa reli ya kisasa na ukarabati wa reli ya kati. Tutaanzisha Usafiri wa treni ya abiria kutoka Dar-Moshi-Arusha,” amesema Majaliwa.

Masanja Kadogosa, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) amesema serikali imetumia Sh. 5.7 bilioni kuirudisha njia hiyo, iliyofungwa kwa miaka 12.

“Mpaka sasa tumetumia Sh. 5. 7 bilioni kuirudisha njia hii, na wahandisi wazawa ndio wamesimamia zoezi hili lote,” amesema Kadogosa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!