Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Majaliwa amtembelea Mbowe hospitalini 
Habari za Siasa

Majaliwa amtembelea Mbowe hospitalini 

Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa (aliyesimama) akimjulia hali Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amemtembelea na kumjulia hali Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe ambaye amelazwa katika hospitali ya Ntyuka jijini Dodoma kwa matibabu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania Chadema, amelazwa hospitalini hapo baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana usiku wa kumakia leo Jumanne tarehe 9 Juni 2020 na kumvunja mguu wa kulia.

Taarifa iliyotolewa na ofisi ya waziri mkuu imesema, Majaliwa amemuombea kiongozi huyo uponyaji wa haraka wa majeraha aliyoyapata.

“Nimepokea kwa masikitiko makubwa  taarifa za tukio la kuvamiwa kwa mheshimiwa Mbowe na watu ambao bado hawajajulikana, namuomba Mwenyezi Mungu amjalie  apone haraka ili aweze kurejea katika majukumu yake,” amesema Majaliwa

Baadhi ya wabunge wa upinzani waliokuwepo hospitalini hapo na ambao walimpokea Waziri Mkuu ni Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya, Mbunge Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!