WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amemtembelea na kumjulia hali Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe ambaye amelazwa katika hospitali ya Ntyuka jijini Dodoma kwa matibabu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania Chadema, amelazwa hospitalini hapo baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana usiku wa kumakia leo Jumanne tarehe 9 Juni 2020 na kumvunja mguu wa kulia.
Taarifa iliyotolewa na ofisi ya waziri mkuu imesema, Majaliwa amemuombea kiongozi huyo uponyaji wa haraka wa majeraha aliyoyapata.
“Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za tukio la kuvamiwa kwa mheshimiwa Mbowe na watu ambao bado hawajajulikana, namuomba Mwenyezi Mungu amjalie apone haraka ili aweze kurejea katika majukumu yake,” amesema Majaliwa
Baadhi ya wabunge wa upinzani waliokuwepo hospitalini hapo na ambao walimpokea Waziri Mkuu ni Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya, Mbunge Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema.
Leave a comment