Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Majaliwa afuta likizo za watendaji Krismas, mwaka mpya kisa… 
Habari za Siasa

Majaliwa afuta likizo za watendaji Krismas, mwaka mpya kisa… 

Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amewaagiza Makatibu Tawala wa Mikoa (RAS) yote nchini humo wahakikishe watendaji wote wa Mikoa, Wilaya, Halmashauri wasiende likizo ya sikukuu ya Krismas na mwaka mpya kwa mwaka huu. Anaripoti Brightnes Boaz, Dar es Salaam … (endelea).

Majaliwa amesema, watendaji wanapaswa kusimamia ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa na madawati na wawe wamekamilisha ifikapo tarehe 28 Februari 2021.

“Suala hili nitalifuatilia mwenyewe ili kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa chaguo la kwanza na la pili wawe wameingia madarasani kufikia Machi Mosi mwaka 2021.”

“Ukamilishaji wa vyumba hivyo pamoja na madawati ufanyike kwa kutumia vyanzo vyenu vya ndani vya fedha,” amesema Majaliwa.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana  Jumatatu tarehe 7 Desemba  2020 alipozungumza na Wakuu wa Mikoa, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Tamisemi.

Kikao hicho ambacho Waziri Mkuu alikiongozo kwa njia ya televisheni akiwa ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma kilihusu upokeaji wa taarifa ya maandalizi ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2021.

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Majaliwa ameiagiza Ofisi ya Rais-Tamisemi ihakikishe kazi hiyo inakamilika kwa wakati  na amewataka watendaji hao wahakikishe ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa na utengenezaji wa madawati unafanyika usiku na mchana.

Awali, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Tamisemi, Gerald Mweri alisema kati ya wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2021, wanafunzi 970 watapangwa kwenye shule maalumu, 1,059 shule za ufundi, 1,280 bweni kawaida, 803,326 watapangwa katika shule za sekondari za kutwa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Juma Homera alisema katika mkoa wake wanafunzi wote waliofaulu watapata nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza 2021 kwa sababu awali walikuwa na upungufu wa vyumba 42 vya madarasa, ambapo wamejenga shule mpya saba zenye vyumba 26 vya madarasa na wamekamilisha maboma 56 na hivyo kuwa na ziada ya vyumba 36 vya madarasa.

Kiongozi huyo alisema, mkoa umeweka mkakati wa kuwapeleka wanafunzi wote waliofeli katika vyuo vya maendeleo ya wananchi ili kuwawezesha kupata stadi za maisha zitakazowawezesha kujitegemea. “Mpango huu tunautekeleza kwa awamu ya pili sasa.”

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi alisema mkoa wake ulikuwa na upungufu wa vyumba 400 vya madarasa, hadi sasa tayari wamekamilisha ujenzi wa vyumba 380 na kwamba watahakikisha hadi tarehe 30 Januari 2021 watakuwa wamekamilisha ujenzi wa vyumba vilivyosalia na wanafunzi wote watachaguliwa katika awamu ya kwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!