Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maharagande ajitosa rasmi ubunge Segerea
Habari za Siasa

Maharagande ajitosa rasmi ubunge Segerea

Spread the love

MBARALA Maharagande, Katibu wa Idara ya Haki za Binadamu Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo, amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Segerea jijini Dar es Salaam, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Maharagande amekabidhiwa fomu hiyo leo Jumatano tarehe 1 Julai 2020 na Athuman Maarufu, Katibu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Jimbo Segerea.

Baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Maharagande amesema, ameanza rasmi safari ya kuliwania jimbo hilo lililokuwa mikononi mwa Chama cha Mapinduzi (CCM), chini ya Bonah Kamoli.

“Safari imeanza rasmi, leo nimechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Segerea katika mchakato ndani ya chama,” amesema Maharagande.

 Chama cha ACT-Wazalendo kimefungua rasmi pazia la uchukuaji na urejeshaji fomu za kugombea urais ubunge, uwakilishi na udiwani leo, ambapo linatarajia kukoma tarehe 13 Julai mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!