Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mahakama yataifisha madini ya mamilioni
Habari Mchanganyiko

Mahakama yataifisha madini ya mamilioni

Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Jijini Dar es Salaam imetaifa madini yenye gramu zaidi ya 800 ya mfanyabiashara Haji Hassan (52) na Jamas Hassan (55). Anaripoti Faki Sosi  …(endelea).

Kutaifishwa kwa madini hayo yenye thamani zaidi ya Sh. Mil 500, ni ni sehemu ya hukumu kwa wafanyabiashara hao walihukumiwa kwenda jela mwaka mmoja au kulipa faini sh. Mil 1, baada ya kutiwa hatia kwa makosa ya kufanya biashara ya madini kinyume cha sheria,

Hukumu hiyo imetolewa leo tarehe 23 Disemba 2020, na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Godfrey Isaya baada ya watuhumiwa hao kukiri makosa yao.

Watuhumiwa hao walishtakiwa kwenye mahakama hiyo kwa makosa ya kuhujumu uchumi pamoja na kufanya biashara ya madini bila kuwa na kibali.

Watu hao walikamatwa wakifanya shughuli hiyo Mtaa wa Lumumba na Uhuru, Kariakoo jijiji Dar es Salaam mapema mwaka huu.

Awali, watuhumiwa hao waliandikia barua kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), kukiri makosa yao na kuomba kufunguliwa pazia la makubaliano.

Katika mazungumzo hayo, walitakiwa kulipa Sh. Mil 40  kama fidia ya makosa hayo ambayo tayari iliishalipwa.

Hakimu Mfawidhi Isaya amesema, madini hayo  yatataifashwa na kwamba, yatakuwa mali ya serikali ambapo mahakama hiyo imemkabidhi Wakili Mwandimizi wa serikali ili akayakabidhi kwenye mamlaka husika.

Watuhumiwa hao wamelipa faini na wameachiwa huru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!