Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama yamuonya Mbowe kwa utoro
Habari za Siasa

Mahakama yamuonya Mbowe kwa utoro

Spread the love

MWENYEKITI wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe amepewa onyo na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kosa la kutohudhuria mahakamani hapo kwa mara mbili. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Onyo hilo limetolewa leo tarehe 31 Julai, 2018 na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri wakati kesi inayomkabili Mbowe na wenzake ilipokuja kwa ajili ya kuwasomea washitakiwa maelezo ya awali.

Hakimu Mashauri amesema iwapo Mbowe atarudia tena kutofika mahakamani kwa sababu zisizo na msingi, dhamana yake itafutwa.

Mbowe ametakiwa na mahakama kuheshimu masharti ya dhamana na kwamba asipofanya hivyo mahakama itamfutia dhamana yake sambamba na kutaifisha fungu la dhamana ambalo ameliweka.

Katika kesi hiyo, Mbowe na wenzake akiwemo Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, Peter Msigwa (Iringa Mjini) na Katibu wa Chadema, Dkt. Vicent Mashinji wanakabiliwa na mashitaka 13 ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki pamoja na kushawishi hali ya kutoridhika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!