Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama Mtwara yamwachia huru Mwambe
Habari za Siasa

Mahakama Mtwara yamwachia huru Mwambe

Spread the love

MAHAKAMA ya Mkoa wa Mtwara leo tarehe 30 Aprili, 2020, imemwachia huru aliyekuwa Mbunge wa Ndanda kwa tiketi ya Chadema, Cecil Mwambe katika kesi ya uchochezi namba 263 ya mwaka 2017 iliyokuwa inamkabili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mtwara … (endelea).

Katika kesi hiyo Mwambe alishitakiwa kwa makosa mawili, kosa la kwanza, kutoa kauli za uchochezi alizotoa katika Kata Reli, wilaya Masasi, huku kosa la pili ni kufanya njama ya kutaka kutenda ovu.

Hakimu Kabate R. ametoa uamuzi huo wa kumwachia huru Mwambe, baada ya upande wa mashataka kushindwa kuthibitisha pasipo shaka kuwa mtuhumiwa alitenda makosa hayo, ambayo pia hayakuleta athari yoyote kwa jamii husika.

Mwambe alifunguliwa kesi hiyo akiwa Mbunge wa Ndanda kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) lakini alijivua uanachama wa chama hicho na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!