MAHAKAMA ya juu nchini Kenya imewaonya wanahabari, mawakili na wahusika wengine wa kesi ya kupinga ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta dhidi ya mpinzani wake, Raila Odinga, anaandika Victoria Chance.
Kenyatta ametangazwa mshindi wa kiti cha urais kupitia chama cha Jubilee huku aliyekuwa mgombea kupitia Muungano wa NASA, Raila Odinga akianguka katika uchaguzi huo na kukimbilia mahakamani.
Mahakama hiyo imewaonya watu wote wanaozungumzia kesi hiyo nje ya mahakama na kwamba masuala ya mahakama yatashughulikiwa na chombo hicho pekee.
Takribani wiki mbili sasa tangu uchaguzi wa Kenya kufanyika ambapo Uhuru Kenyatta (JUBILEE) aliibuka mshindi dhidi ya mpinzani wake Laila Odinga (NASA), huku nyuma ya pazia ikisemekana kuwa
Uhuru Kenyatta kapata ushindi kwa njia isiyo sahihi hivyo suala hilo kufunguliwa mashtaka katika mahakama ya juu nchini Kenya.
Agizo hilo limetolewa na mahakama huku hatua mbalimbali za kesi hiyo zikiendelea ambapo mapema jumatano ya wiki hii mawakili watakaoiwakilisha Tume ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya (IEBC) wanaoongozwa na Poul Nyamodi na Kamau Karori wamekabidhiwa nakala za stakabadhi zote za uchaguzi tayari kwa kujibu malalamiko na wale wa Uhuru Kenyatta kupitia kampuni ya uwakili ya Otachi na Ogeta wanatakiwa kuandaa majibu ya malalamiko.
Kesi hiyo inatarajiwa kushika kasi wiki ijayo baada ya kikao kitakachojadili jinsi ya kuishughulikia kesi hiyo.
Leave a comment