Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli: Nitaendelea kuwaamini wanawake 
Habari za Siasa

Magufuli: Nitaendelea kuwaamini wanawake 

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli amesema, Serikali anayoiongoza itaendelea kuwaamini wanawake katika nafasi mbalimbali za uongozi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Ijumaa tarehe 13 Novemba 2020 wakati akihutubia na kufungua Bunge la 12 jijini Dodoma.

Ameanza hotuba yake kwa kutoa shukurani kwa uongozi wa Bunge ukiongozwa na Spika Job Ndugai kwa kuchaguliwa na wabunge kuendelea kuwa Spika wa Bunge hilo kwa miaka mitano mingine “hongera sana.”

Ndugai ambaye ni Mbunge wa Kongwa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) amechaguliwa kuwa Spika kwa Bunge hilo la 12 akiendelea na nafasi hiyo aliyokuwa nayo Bunge lililopita la 11.

“Nampongeza pia Dk. Tulia Ackson kwa kuchaguliwa kwa mara nyingine kuwa Naibu Spika; tena mara hii akiwa Mbunge wa kuchaguliwa kutoka Jimbo la Mbeya Mjini.”

Makamu wa Rais, Samia Suluhu

“Hongera sana Dk. Tulia. Huu ni uthibitisho kwamba, nchi yetu, kupitia Serikali inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi, inawaamini sana wanawake,” amesema Rais Magufuli huku akishangiliwa na wabunge.

Rais Magufuli amesema, “kama mnavyofahamu, Makamu wetu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, naye ni mwanamama. Aidha, Bunge hili la 12 nalo lina wabunge wengi wanawake.”

“Kwa msingi huo, napenda nitumie fursa hii kuahidi kuwa, Serikali ninayoingoza, itaendelea kuwaamini wanawake katika kushika nafasi mbalimbali za uongozi. Wanawake na akinamama Oyee!!!,” amesema Rais Magufuli na kuibua shangwe bungeni.

Dk. Tulia Ackson, Naibu Spika

Pia, Rais Magufuli amewapongeza wabunge wote kwa kuchaguliwa kuwa wabunge wa Bunge hilo la 12.

“Mmechaguliwa kwa vile wananchi wana imani kuwa mna uwezo wa kuwawakilisha vizuri. Hivyo basi, nawasihi msiwaangushe wananchi waliowachagua. Watanzania wana imani kubwa sana na Bunge hili,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!