Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli awahoji wanaotaka akae madarakani miaka mitano
Habari za Siasa

Magufuli awahoji wanaotaka akae madarakani miaka mitano

Rais John Magufuli, mgomba Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM
Spread the love

MGOMBEA urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli amewahoji wananchi wanaotaka akae madarakani muhula mmoja tofauti na walivyokaa marais waliopita. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Rais wa awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere alikaa madarakani zaidi ya miaka 20 huku waliomfuata Dk. Ali Hassan Mwinyi (awamu ya pili), Benjamin Mkapa (awamu ya tatu) na Jakaya Kikwete (awamu ya nne) waliongoza miaka 10 kila mmoja ambayo ni sawa na mihula miwili.

Rais Magufuli aliyeingia madarakani tarehe 5 Novemba 2015 amesema, kwa nini watu hao wanataka wampunzishe ilihali amekaa madarakani miaka mitano.

Akizungumza na wananchi wa Jimbo la Chemba mkoani Dodoma leo Jumatatu tarehe 26 Oktoba 2020, amewaomba Watanzania wamchague tena akamilishe miaka yake 10.

“Nyerere alikaa miaka 20 na kitu, alitutafutia uhuru akang’atuka mwenyewe, akaja Mzee Mwinyi akakaa miaka 10 akaondoka, marehemu Mkapa kakaa miaka 10 akapumzika, akaja Kikwete amekaa miaka 10 akampumzika, mimi nimekaa miaka mitano mnataka mnipumzishe.”

Rais John Magufuli akizindua kitabu cha Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, wengine ni wastaafu, Jakaya Kikwete na Ali Hassan Mwinyi

“Mtanipa miaka mitano mingine nifikishe kumi kama wenzangu,” amewahoji wananchi hao ambao walimuahidi kumchagua.

Rais Magufuli amewaahidi wananchi wa Chemba na Watanzania kwa ujumla akichaguliwa kuwa Rais wa Tanzania ataongeza kasi ya utatuzi wa changamoto zao sambamba na kuwaletea maendeleo.

Aidha, amewasihi Watanzania kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani, ikiwa sambamba na kurudi nyumbani baada ya kupiga kura Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!