Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Magufuli athibitishwa kwa asilimia 100 kugombea urais Tanzania
Tangulizi

Magufuli athibitishwa kwa asilimia 100 kugombea urais Tanzania

Spread the love

WAJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamemthibitisha Dk. John Pombe Magufuli kuwa mgombea Urais wa Tanzania kwa asilimia 100 katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Shughuli hiyo ya upigaji kura imefanyika leo Jumamosi tarehe 11 Julai 2020 jijini Dodoma.

Akitangaza matokeo hayo, Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema, wajumbe wa mkutano huo ni 1822 na waliopiga kura walikuwa 1822.

Spika Ndugai amesema, hakuna kura hata moja iliyoharibika.

Amesema, kura halali zilikuwa 1822, “kura halali ni 1822. Kura za ndiyo ni 1822 ambayo ni sawa na asilimia 100 ya kura zote. Hakuna kura ya hapana.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!