Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli ateua wabunge 2
Habari za Siasa

Magufuli ateua wabunge 2

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS Tanzania, John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Novemba, 2020 amefanya uteuzi wa wabunge wawili wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kwanza, Rais Magufuli amemteua Humphrey Polepole kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Polepole ni Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Pili, Rais Magufuli amemteua Riziki Said Lulida kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM

Katika Bunge la 11 lililomalizika, Riziki alikuwa mbunge wa viti Maalum kupitia Chama Cha Wananchi (CUF) ambaye mwishoni mwa Bunge hilo, alitangaza kutimkia Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikuku imesema, wabunge wateule hao wataapishwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1 Comment

  • Asante ndugu jpm kwa uteuzi wa pole pole fikra zako na uteuzi uo zimeunga na wana ccm na taifa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!