Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli atangaza Dodoma kuwa jiji
Habari za SiasaTangulizi

Magufuli atangaza Dodoma kuwa jiji

Spread the love

RAIS John Magufuli jana katika sherehe za Muungano, ametumia sherehe hizo kutangaza Dodoma kuwa jiji badala ya kuwa Manispaa na kumtangaza aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma, Godwin Kunambi na kuwa Mkurugenzi wa Jiji. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Mbali na kutangaza kuwa Dodoma ni Jiji ametangaza vita kwa mtu au kikundi chochote kitakachojaribu kutaka kuvunja au kuruvuga Muungano kuwa yeye (Magufuli) pamoja na rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kuwa watamshughulikia kwa gharama yoyote.

Akihutubia umati wa watu Mafufuli alisema kuwa licha ya kuwa siku ya leo (jana) siyo siku ya hotuba bali ni siku ya sherehe alisema kuwa hatahakikisha analinda muungano kwa gharama yoyote na atakayejaribu kutaka kuvunja muungano huo atashughulikiwa kwa nguvu zote.

Alisema kuwa serikali anayoiongoza haitamfumbia macho mtu yoyote awe wa ndani ya nchi au nje ya nchi ambaye atajaribu au kutaka kuvuruga muungano ambao umeasisiwa na viongozi waliokuwa marais wakati huo kwa maana ya Juliasi Kambarage na Abeid Amani Karume.

“Mtu yoyote sichezee Muungano, Mimi na Dk. Shein tutahakikisha tunalinda Muungano kwa gharama yoyote, Muungano wetu ndiyo ngao yetu kamwe hatutamwonea aibu mtu yoyote atakaye jaribu kuchezea Muungano wetu,” alisema Dk. Magufuli.

Akizungumzia changamoto mbalimbali za Muungano alisema kupitia kwa makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan changamoto nyingi za mashirikiano zimepungua kutoka 22 hadi kufikia 11.

Alisema kutokana na hali hiyo alisema Muungano uweweza sauti hata kimataifa na ni kati ya muungano uliodumu kuliko nchi nyingine ambazo zilikuwa na muungano .

Alisema Juhudi za Muungano zimeweza kuwa mkombozi wa utatuaji wa migogoro katika maeneo mengi Tanzania bara na Visiwani huku akieleza kuwa muungano ni lazima ueshimiwe na kulindwa kwa gharama yoyote.

Dodoma kuwa Jiji

Akizungumzia Dodoma kuwa jiji alisema kuwa amejaribu kuangalia maeneo mbalimbali ambayo ni majiji na kubaini kuwa lipo jiji la Dar es salaam, jiji la Tanga, Jijij la Mbeya, Jiji la Mwanza na kutafakari na kuona kama anayo mamlaka ya kufanya jambo lolote na kueleza kuwa ameweza kujiridhisha na kuamua kutangaza Dodoma kuwa Jiji badala ya kuendelea kuwa Manispaa.

“Nimejaribu kuangalia majiji yaliyopo nikaona kuna jiji la Dar es salaam, jiji la Tanga, Jijij la Mbeya, Jiji la Mwanza,na kwammlaka niliyonayo kuanzia leo natangaza kuwa Dodoma siyo Manispaa tena bali linakuwa jiji na kuanzia leo tarehe 26 mwezi huu na mwaka huu aliyekuwa mkurugenzi wa Manispaa atakuwa mkurugenzi wa Jiji la Dodoma” alisema Dk. Magufuli.

Alisema kutokana na Dodoma kuwa jiji baada ya sherehe za Muungano atakwenda kukutana na rais wa Benki ya Maendeleo ili aweze kumchomekea kwa ajili ya kupata hela za kufanya miradi ya maendeleo kwa bajeti ya jiji badala ya kupata pesa za miradi yenye sura ya Manispaa.

Uchumi kukua 

RAIS Dk. Magufuli alisema kuwa kwa sasa serikali awamu ya tano inaendelea kupambana na kuhakikisha inafanya vizuri ikiwa ni pamoja na kupandisha uchumi wan chi.

Alisema kuwa kwa sasa uchumi umekua kwa asilimia 7 na anategemea baada ya mwaka mmoja uchumi utaendelea kukua hadi kufikia asilimia 7.1 huku akisema hata ali ya kiafya imeimarika ikiwa ni pamoja na kupambana na hali ya malaria kushuka kutoka asilimia 14.3 hadi kufikia asilimia 7.3.

Viongozi washindwa kufika 

Pamoja na kusherehe hizo kupambwa na maonesho mbalimbali lakini baadhi ya viongozi mbalimbali hawakuweza kufika katika sherehe hizo licha ya kutotangazwa sababu yoyote licha ya kuwa ni lazima wafike au wasifike katika sherehe hizo.

Viongozi ambao hawakufika katika sherehe hizo ni pamoja na Rais wa awamu ya pili All Hasani Mwinyi, Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, mawaziri wastaafu ni Mizengo Pinda, Dk. John Malecella, Edward Lowasa huku rais wa awamu ya tatu William Mkapa akiwa ni kati ya viongozi wastaafu waliohudhuria sherehe hizo.

RC Dodoma

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dk. Binilith Mahenge alisema kitendo cha Manispaa kuwa jiji kitaongeza ari ya kimaendeleo lakini pia ni hshima kwa wakazi wa Dodoma.

Akizungumza na waandishi wa habari katika mahojiano maalum alisema wanchi wa Jiji la Dodoma wanatakiwa sasa kujituma kufanya kazi ili kuweza kujiongezea kipato na kubadilika na kuona kuwa sasa wanatakiwa kubadilisha mfumo wa maisha na kuishi katika mfumo mwingine.

Mbali na hilo alisema hata hivyo serikali ya mkoa inaro jukumu zaidi katika kuhakikisha inasimamia miundombinu mbalimbali pamoja na mipango ya kimaendeleo ili kukithi mahitaji ya wananchi ambao wanaishi katika jiji la Dodoma.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa

Naye aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa na sasa kupandishwa hadhi kuwa jiji Godwini Kunambi alisema kitendo cha Manispaa kuwa jiji kinapelekea zaidi kuendelea kutekeleza mipango kabambe ili kuweza kukidhi matakwa ya jiji.

Alisema pamoja na mambo mengine lakini kwa sasa wakati ikiwa Manispaa aliweza kufanya makusanyo kuwa na kiwango cha juu hadi kufika asilimia 66 ambapo alitakiwa kukusanya asilimia 50.

Alisema kuwa katika manispaa pekee Tanzania ambayo inamzidi kwa makusanyo ni manispaa ya Ilala wakati yeye akiwa anamakusanyo akubwa zaidi .

Alisema kitendo cha manispaa kuwa makao jiji itawafanya wananchi kuhakikisha wanafanya kazi ya kujipatia kipato kama pale wataweza kufanya mambo mbalimbali kwa ajili ya kujiongezea kipato cha mtu mmoja mmoja.

Wananchi 

Baadhi ya wananchi ambao waliozungumza na gazeti hili alisema kitendo cha Manispaa kutangazwa kuwa jiji kitasaidia sana wananchi kujiongeza na kufanya shughuli za kimaendeleo na kuachana na tabia za kubweteka.

Mmoja wa wananchi ambaye pia ni mjasiliamali Lilian Sambu, alisema kuwa kila mtu sasa ataweza kupata fursa ya kuongeza juhudi katika ufanyaji wake wa kazi sambamba na kuboresha shughili anazozifanya.

“Kuna watu ambao wanaweza kubeza kuwa Manispaa hajafikia kiwango cha kuitwa jiji lakini kama hautaweza sasa na kuanza kuzoea lini tutaweza kuanza na kuzoea,” alihoji Lilian

Katika hatua nyingine mjasiliamali huyo aliwataka wananchi ambao ni wajasiliamali wenzake kuhakikisha wanafanya shughuli zao kwa viwango na ubora ambao unakubalika kwa kuzingatika kuwa kwa sasa jiji la Dodoma litakuwa na wageni wengi na waaina mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!