RAIS wa Tanzania, John Magufuli amemteua Balozi John Kijazi kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema, uteuzi wa Balozi Kijazi ambaye ni ni Katibu Mkuu Kiongozi unaanza leo Ijumaa tarehe 21 Agosti, 2020.
Balozi Kijazi anachukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Hayati Benjamin William Mkapa.
Soma zaidi:-
Mkapa alifikwa na mauti Alhamisi ya tarehe 23 Julai 2020 saa 3:30 usiku katika moja ya Hospitali ya jijini Dar es Salaam kwa mshituko wa moyo.
Leave a comment