Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli ampongeza Rais mpya wa Malawi
Habari za Siasa

Magufuli ampongeza Rais mpya wa Malawi

Lazarus Chakwera, Rais wa Malawi
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amempongeza Dk. Lazarus Chakwera kuwa Rais mpya wa Malawi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Chakwera amechaguliwa na Wamalawi katika uchaguzi wa marudio uliofanyika tarehe 23 Juni 2020 kwa kupata asilimia 58 akimshinda Rais aliyekuwa madarakani Peter Mutharika.

Uchaguzi huo ulifanyika baada ya ule wa awali wa Mei 2019 kufutwa na mahakama Februari 2020 baada ya kubaini ulikuwa na dosari.

Soma zaidi:-

Dk. Chakwera aliwasilisha maombi hayo mahakamani yaliyompa ushindi na katika uchaguzi wa marudio, aliwakilisha vyama zaidi ya vitano vya upinzani vilivyomng’oa Mutharika.

Tarehe 28 Juni 2020, Dk. Chakwera aliapishwa kuwa Rais wa Malawi.

Leo Jumatano tarehe 1 Julai 2020, Rais Magufuli ametumiw akaunti yake ya kijamii ya Twitter kumpingeza Rais Chakwera.

Rais Magufuli amesema, “Nakupongeza Dkt. Lazarus Chakwera kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Malawi.”

“Kwa niaba ya Serikali na Watanzania wote, naahidi kuendeleza uhusiano wetu wa kidugu, kirafiki na ujirani mwema hususani katika masuala ya uchumi na ustawi wa jamii. Hongera sana Mhe. Rais,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!