Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli ajiapiza ‘kuwamaliza’ Mdee, Bulaya
Habari za Siasa

Magufuli ajiapiza ‘kuwamaliza’ Mdee, Bulaya

Wabunge Ester Bulaya na Halima Mdee
Spread the love

RAIS John Magufuli, amempongeza Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua dhidi ya wabunge “wasumbufu” na kuahidi kuwashughulikia zaidi watakapokuwa nje ya Bunge, anaandika Charles Willliam.

Rais Magufuli ameyasema hayo, Ikulu jijini Dar es Salaam alipokuwa akipokea ripoti ya usafirishaji wa mchanga wa dhahabu – maknikia ambapo amedai kuwa wapo wabunge wanaotumia vibaya kinga yao na kwamba yeye atawachukulia hatua zaidi baada ya kufukuzwa bungeni.

“Mheshimiwa Spika endelea hivyo hivyo kule bungeni, wafukuze waropokaji wote ili wakose pa kuropokea na wakija kuropoka huku nje tutawashughulikia kwasababu wakiwa ndani ya bunge wanakuwa na kinga,” amesema na kuongeza;

“Wakishakuwa huku nje na wakaropoka mimi nakuahidi, I will deal with them (nitashughulika nao).”

Kauli ya Rais Magufuli ni kama msumari wa mwisho kwa wabunge Halima James Mdee wa Kawe na Ester Amos Bulaya wa Bunda Mjini – wote Chadema, ambao wamefungiwa kushiriki vikao vya Bunge mpaka mwakani kutokana na kudaiwa kudharau kiti cha Spika.

Adhabu hiyo kwa Mdee na Bulaya inafuatia mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Bunge ya Kinga, Haki na Maadili ambayo yalipata Baraka za wabunge walio wengi pamoja na kiti cha Spika.

Katiba ya Tanzania Ibara 101 inawalinda wabunge kutohojiwa wala kuchukuliwa hatua nje ya Bunge kutokana na kauli wanazozitoa ndani ya Bunge, kauli ya Rais kuwa atawashughulikia wabunge wanaofukuzwa bungeni inalenga kuwapa wakati mgumu Mdee na Bulaya.

Tayari wabunge hao wametangaza kuliburuza mahakamani Bunge, wakipinga kufukuzwa pasipo kuhojiwa wala kusikilizwa. Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema amethibitisha kuwa hatua za kulifikisha mahakamani Bunge zinaendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!