Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli aahidi kusimamia sekta ya madini
Habari za Siasa

Magufuli aahidi kusimamia sekta ya madini

Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, John Magufuli akihutubia mkutano wa kampeni Shinyanga
Spread the love

JOHN Magufuli, Mgombea Urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameahidi kuimarisha mifumo ya kisera na kisheri kwenye sekta ya madini ili Watanzania wote wanufaike na rasmiliamli hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Shinyanga … (endelea).

Rais Magufuli ametoa ahadi hiyo leo Alhamisi tarehe 3 Septemba 2020 wakati akinadi Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020/25 katika mkutano wa kampeni za Urais mkoani Shinyanga.

Amesema mabadiliko hayo yatawawezesha Watanzania kunufaika na utajiri wa madini, kwa kuwa watapewa kipaumble katika shughuli za uchimbaji madini.

Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, John Magufuli akihutubia mkutano wa kampeni Shinyanga

“Ukurasa wa 105 unazungumzia juu ya masuala ya madini, kuimarisha mifumo ya kisera na kisheria ili kuwezesha wananchi wa Taifa kwa ujumla kunufaika na utajiri wa madini na rasilmali zao.”

“Tunataka madini haya yawanufaishe, ndio maana tunaruhusu wachimbe wenyewe,” amesema Magufuli.

Wakati huo huo, Magufuli ameahidi kuboresha sekta ya kilimo mkoani Shinyanga na Tanzania kwa ujumla, ikiwemo kutekeleza ujenzi wa viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo .

“Katika ukurasa wa 44 wa Ilani ya CCM, unazungumzia juu ya kujenga vituo vya kuchakata na kuhifadhi mazao katika mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Geita, Iringa, Kagera, Manyara, Mara Mbeya, Tabora, Morogoro, Mtwara na Shinyanga,” ameahidi Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!