Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Madiwani wa CCM wamsusia Meya kikao
Habari za Siasa

Madiwani wa CCM wamsusia Meya kikao

Baraza la madiwani Manispaa ya Iringa wakiwa kikaoni
Spread the love

MADIWANI wa CCM katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wamegoma kushiriki kikao cha baraza la madiwani kilichotarajiwa kufanyika leo tarehe 7 Novemba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mkurugenzi wa Mansipaa ya Iringa Mjini ambaye ni Katibu wa kikao hicho, Hamid Njovu ameahirisha kikao hicho hadi tarehe 14 Novemba mwaka huu.

Madiwani wa Chadema ndio waliofika kwa ajili ya kushiriki kikao hicho, lakini idadi ya akidi haikutimia na kupelekea kikao hicho kutofanyika.

Kufuatia mgomo huo, Mwenyekiti wa CCM wilayani Iringa, Said Rubeya amesema madiwani wa CCM wako sahihi kutoshiriki kikao hicho, akisema kuwa meya wa manispaa hiyo, Alex Kimbe (Chadema) alikiuka kanuni.

Rubeya amedai kuwa, katika kikao cha CCM madiwani wa chama hicho walilalamikia ubabe wa meya huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!